Saturday, January 13, 2007

Ibada za Kikoloni


Tunaendela kusali ibada za kikoloni

Na Nyasigo Kornel

WASOMI na watawala wetu wamekuwa wakimkejeli Chifu Magungo wa Usagara kwa kile kinachoitwa kutia sahini mkataba wa ulaghai wa kuwapa wakoloni ardhi kwa muda wa maika 999 chini ya mpelelezi Dk. Karl Peters.

Chifu Magungo analo la kujitetea, anaweza kusema kuwa hakuwa na elimu, taarifa na maharifa ya kutosha juu ya mikataba na dhana nzima ya ukoloni.

Hata katika miaka hii ambapo wasomi ndio wamekuwa watawala wan chi hii, bado tunaona mikataba kama hii ya Chifu Magungo zikiendesha.

Zimekuwa zikiingia ndani ya nchi kama makampuni, asasi au madhehebu za kididni.

Ukisoma kitabu cha ‘The Black Batch’ kilicholeta ugomvi na kuzua mjadala mkubwa mwishoni mwa karne iliyopita huku ikilaumiwa na wasomi wa nyakati hizo kuwa kimemtukana mwafrika, utaona jinsi gani wazungu wanavyotuona kama makatuni katika fikara zetu.

Kitabu hicho kinalaumiwa kwa kuandika siri na namna ya kumtawala Mwafika huku kikitumiwa na shirika la kijasusi la CIA kwa ajili ya kuwageuza wasomi wetu mabumbumbu wao.

Kitabu hicho kinasema, “Ni rahisi sana kumtawala msomi wa Kiafrika kuliko mwafrika asiye na kisoma, na kwa sababu mwafrika asiye na kisomo anamwamini nduyu yake aliyesoma, basi jitahada kubwa ya Mmarekani na wenzake iwe ni kuwanywesha kasumba.”

Sijui ni kwa nini wanapanafrikanizism walikichukia hiki kitabu na kukipigia kelele kuwa wamedharahuliwa wakati kilielezea ukweli kabisa.

Katika kitabu cha Prof Eduard Achermann kiitwacho ‘Cry Beloved Afrika’ au kwa kiswahili ‘Fumbuka Afrika’ anasema kuwa ilifikia hatua ndugu zetu, tena waliokuwa wapigania uhuru na demokrasia ya Afrika kama marehemu Mobutu Seseseko aliyekuwa rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, alikuwa hajui utaofauti kati ya akaunti yake na akaunti ya taifa.

Anasema hata rais Kerekou wa Benin alidhani Benki ya serikali ni mali yake binafsi.

Katika gazeti la wafanyabiashara iitwayo ‘Bilanz’ ambayo ilionyesha wapi mameneja wanalazima kuwapa rushwa wataalamu na kiasi gani ili waweze kupata mikataba, ramani hiyo iliyonyesha bara la Afrika.

Kitabu hicho kinasema kinanukuu wamisionari wa kizungu waliofikiri kuwa kwa kumsomesha mwafrika watawasaidia ndugu zao, wanasikitika kuwa kumbe walikosea, kwa maana walijikuta wakiwa wameunda wataalamu ambao waliwageukia ndugu zao na kujiunga na makampuni ya dunia ya kwanza na kutupora mali zetu.

Wiki hii tumemsikia Mh. Andrew Chenge akitutuliza Watanzania, akisema kuwa tusiwe kama Waingereza wanaouliza kuhusu rada tuliouziwa kwa bei ya kuruka, na hata kuwmeka Tonny Blair katika wakati mgumu.

Waingereza wameona kabisa kuwa sisi hatuna uwezo wa kuiuliza serikali zetu na kuiwajibisha juu ya mikataba mibovu wanayoifanya na makampuni ya nje.

Kinyume chake huku kwetu Bunge letu liko kimya, kwao hilo sio tatizo la kujadili. Bunge letu limekuwa kama vilabu vya mashoga‘gays clubs’ za Amerika ambapo ukifika unawakuta wanaume wasafi wakiwa wamevalia suti utadhani wanazungumzia biashara kubwa kubwa au hoja nzito za maendeleo, kumbe hamna lolote.

Bunge liko tayari kutumia siku kujadili kuhusu joho la Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano. Huyu akitaka iwe na picha ya hiki na mwingine akitaka iwe mpya ili mradi siku ipite.

Ilipofikia suala wananchi kutaka kujua juu ya ukweli kuhusu tuhuma za ufujaji wa pesa za wananchi kunua maghala ya ‘Quality Group’ Spika alisema hayo ni ya mahakama, wao wako bize wanajadili kuhusu joho la Spika.

Katika dunia ya leo ya Mtanzania, amejengewa akilini kuwa hawezi, tena kila anachokifanya akiwezi kufanikiwa. Na aliyetujengea mawazo hayo ni Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa.

Hili lilionekana katika mwenendo mzima wa uwekezaji, huku akibeza kwenye vyombo vya habari kuwa sisi hata tukiachiwa miradi hatuwezi.

Huyu Benjamin Mkapa ni mmoja wa matunda ya Pan-Afrikanism, wale watu waliokuwa wakitaka Waafrika wajikomboe, wajitambue, wajiamini na wawe tayari kulinda nchi zao.

Kumbe zile zilikuwa ni gia za Waafrika wasomi wa enzi hizo kunyemela madaraka mara baada ya mkoloni kutoka.

Kwani walipopata madaraka, katika baadhi ya wananchi walitamani mkoloni arudi, ndugu zao hawakujali kuwajengea mazingira ya uhuru kamili.

Mheshimiwa Idd Simba alipoongelea suala la ‘uzawa’ aliambiwa kuwa neno hilo halipo katika kamusi ya utandawazi.

Watu wenye akili kabisa walionekana kumpinga bungeni, kumbe wamejificha nyuma ya utandawazi ili watumie makampuni ya nje kutunyonya jasho la wananchi.

Mwalimu Nyerere alikuwa akiwaimbia hawa viongozi tulionao sasa hivi kuwa ‘pesa sio msingi wa maendeleo’. Inawezekana hawakuwa wanamwelewa kabisa, na pengine wengine walikuwa wakimwogopa kwa unafiki tu. Kwani hata baada ya kufa kwake watu wachache wanaoonekana kujua falsafa zake.

Leo hii utasikia wananchi wanashangilia kuona uhusiano mzuri wa Rais wa nchi yetu na Rais wa Marekani. Kwani hata kwenye vyombo vya Habari utaona katika kurasa za mbele zikiwa zimeandikwa ‘Bush akubali kuisaidia Tanzania’. Tunashangilia misaada na kuyakimbilia kumbe yanatuweka kuwa tegemezi.

Taratibu tutaanza kumchagua rais aliye na uwezo mkubwa wa kuombaomba. Lakini pesa hizi za misaada inatolewa katika maeneo ambayo hayatusidii.

Sasa hivi baadhi ya viongozi wetu hawana muda tena wa kutembelea wananchi, wanatafuta pesa kwa wahisani, wanafikiri nchi itaendelea kwa misaada. Maendeleo makubwa ya kwanza ni kubadili fikra za wananchi wako na kuwaambia kuwa wanaweza sio kuwatukana tena wazi kwenye vyombo vya habari kama alivyokuwa akifanya ndugu yetu mstaafu.

Juzi hapa nilipeleka makala yangu kwenye gazeti moja kubwa la kiingereza linalotoka kila siku, makala ilikuwa inazungumzia sera za Mwamerika, lakini haikutolewa.

Mhariri wa gazeti hilo alinitumia barua pepe na kuniambia kuwa hataki makala inayompinga George Bush na Rais Kikwete.

Mhariri huyo mwanamke alisema, “Rais wetu juzi alishikana mkono na Bush, sasa hivi Bush ni rafiki yetu, na tuko mbioni kufaidi misaada ya Amerika, hatutaki makala yanayowapinga kwa wakati kama huu ambapo tunaweza kutengeneza opportunities.”

Watanzania wengi bado tupo kama huyu mhariri. Hawa ndio wale ambao Plato, mwanafalsafa wa enzi za kati aliwaiita Doxa ‘watumwa wa mawazo’ ambao wanakodoa macho kwenye kivuli cha mwanga wakidhani ndio mwanga halisi.

Sasa nitumie makala hii kumjulisha kuwa maembe anayokupa mzungu sio ile unayohihitaji bali ni ile ilijaa hamira, na haishibishi.

Serikali za Ulaya na Amerika hao tunowashangilia kama Miungu watu, wanathamini na kujali ng’ombe wake mmoja kuliko maisha ya mwafrika mmoja.

Sasa hivi ripoti ya Benki ya Dunia inasema kuwa ng’ombe mmoja wa Ulaya analipwa ruzuku ya dola za Kimarekani 2 kwa siku na wanataka kuongeza zaidi, huku ng’ombe mmoja wa Japani anatolewa ruzuku ya dola za Kimarekani 4.

Hii ni zaidi ya mara mbili ya pato la Mwafrika ambao asilimia zaidi ya 40 uishi kwa chini ya dola moja kwa siku.

Mara nyingi hutoa mabilioni ya pesa sio kusaidia kilimo, kutafuta masoko, kujenga miundombinu vijijini na kutoa elimu bora.

Utaona pesa nyingi zinakuja ndani ya nchi kuzuia ukeketaji wa wanawake (Female Genital Mutilation - FGM), wakisema kuwa mwanamke hatendewi haki.

Kuna vikwazo vikubwa vinavyomkumba mwanamke na hasa wa vijijini kuliko swala hili la kukeketa. Inakadiriwa kuwa dola za Kimarekani trilioni 9 tu zikitumiwa vizuri, ingeweza kukwamua asimilia 80 ya wanawake kutoka katika umaskini uliokithiri.

Amerika inatumia kiasi hicho hicho cha dola trilioni 9 kwa mwaka kwa kununulia tiketi za kuingia kuangalia picha za sinema kila mwaka.

Katika Ripoti ya Dunia Kuratibu Misaada (Global Aid Monitoring Report) ilisema kuwa nchi za Afrika zimeshapata zaidi ya dola za Kimarekani trilioni moja kuzuia ukeketaji.

Kiasi hiki cha pesa ni mara nne ya misaada ya elimu kwa nchi za Afrika ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya taifa lolote.

Pesa nyingi zimetumika kuzuia suala la adhabu mashuleni. Wabunge wanatumika kutunga sheria hizi ambazo watu walio nyuma ya hizi sheria wamepewa mabilioni ya pesa.

Watoto haohao, ambao wazungu na asasi zao hizo wanaojifanya kuwahurumia kuwa wanachapwa viboko na adhabu mashuleni wana shida nyingi za muhimu kuliko viboko.

Utamkuta huyo mtoto hana sare za shule, hana uhakika wa kula chakula, hana madaftari na ana magonjwa yanayotibika ila huduma za afya ni mbovu.

Mtoto huyu huyu anayemhurumia anafika darasa la saba bila kuchapwa viboko anafaulu na hawezi kujilipia karo. Sasa kumtetea kwako kwenye viboko vimemsaidia nini?

Tunataka mtoto wa kitanzania aishi kama mtoto wa Swedeni na Norway, ambaye hachapwi viboko shuleni. Wakati mazingira ya mtoto wa Swedeni ni tofauti kabisa na huyu mtoto wa kitanzania.

Kuna haja gani kujifanya kuwa tunawahurumia watoto wetu kwa kutandikwa fimbo mbili nali hatuwahurumii kwa kulala njaa na kushindwa kuendelea na shule?

Hivi karibuni kuna makabila yalikataa kushurutishwa kuacha kukereketa wanawake na wakakataa.

Hata mimi, nawaunga mkono jamii hizo kwa kukataa. Hawaoni sababu ya wewe kumwonea huruma juu ya kile anachokipenda yeye na anakifanya kwa hiari, tena ikiambatanishwa na sherehe.

Leo hii eti atokee mtu kutoka mjini, yaani msomi, anajifanya anahuruma, wanaowaonea wanawake uchungu eti kwa sababu sehemu yao ya mwili umekatwa. Maskini jeuri… hawawaelewi.

Jamii inaongea taratibu (society speaks silent), kwa maana nyingine ni kuwa mbinu wanazotumia asasi hizi sio sahihi. Wanawapa wananchi wasichotaka kula na kuwanyima wanachokihitaji.

Katika ripoti ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere iliyojumuisha maoni ya wananchi juu ya kile wanachokihitaji kwanza ili waendelee. Wananchi waliorodhesha mabo yafuatayo kwa mtiririko; Elimu, kilimo, afya, usafiri, maji, utawala bora na ajira.

Wazungu hawatakupa pesa katika sekta hizi na hata wakikupa wanafadhili mradi usio endelevu. Na kibaya zaidi ni pale wasomi wetu ambao wangejitahidi kufanya hii miradi inufaishe taifa huwa upeo wao unakoma pale ambapo pesa za wahisani zinapoisha.


Email: emmakornel@yahoo.com
Cellular: 0715 551455


1 comment:

musa said...

Makala nzuri sana hii. Nimeikubali